Wana vyuo watahadharishwa na matumizi ya mitandao


Mkurugenzi Msaidizi wa usalama mtandao kutoka Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,Mhandisi Stephen Wangwe,akizungumza leo jijini Arusha.


 

Bertha Mollel , Arusha.

 

Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wamawatahadharisha wana vyuo kuwa makini na matumizi ya mitandao ikiwemo kujiridhisha na madhumuni ya kila wanachotaka kuchapisha  ili kujikinga na uhalifu  sambamb na dhima za udhalilishaji, utapeli na udukuzi wa taarifa binafsi.

 

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Usalama Mtanda kutoka , Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari , Mhandisi Stephen Wangwe, kwenye semina ya kuwajengea uelewa wanafunzi na Menejimenti ya Chuo cha Ufundi Arusha (ATC),kuhusu usalama mtandao.

 

Alisema kuwa Udhalilishaji mtandaoni,utapeli na udukuzi wa taarifa binafsi zimekuwa miongoni mwa changamoto za kimtandao hapa nchini hivyo ni vema watumiaji wa mtandao kuwa makini kabla ya kuchapisha jambo lolote ili kujikinga na matukio hayo.


"Kimsingi hili ni janga la dunia na hapa nchini maeneo matatu yamekithiri sana la kwanza ni udhalilishaji mtandaoni hili tumeliona likikua kwa kasi sana,kunyang'anywa akaunti ambapo wamekuwa wakiombwa taarifa zao kumbe sio kwa watoa huduma na la tatu ni utapeli kuna zile meseji maarufu ile hela tuma kwenye namba hii,siku hizi wengine wanajifanya waganga,"amesema

 

Amesema lengo la mafunzo hayo ni kupunguza matukio ya uhalifu mtandaoni kwa kujenga uelewa kuhusu mbinu zinazotumika kufanya uhalifu mtandaoni, namna wanavyoweza kubaini mashambulizi ya mtandao na masuala gani wanayoweza kufanya ili kujikinga dhidi ya uhalifu wa mtandao.

 

Amesema serikali ina mkakati wa taifa wa elimu kwa umma wa usalama mtandao ambapo wanatarajia kufikia makundi mbalimbali ikiwemo vijana,wazee na makundi ya wenye mahitaji maalum wakiwemo watu wenye ulemavu na kuwa watawaandalia maudhui maalum ili elimu ya kujikinga mtandaoni iwafikie wote.

 

 

Kwa upande wake Mkuu wa ATC, Musa Chacha, alisema kutokana na umuhimu wa mafunzo hayo,kupitia idara yao ya Tehama wataongeza suala la usalama mtandao na kufundisha wanafunzi wao kwenye masomo ya kawaida.

 

"Mafunzo haya ni muhimu  sana na  sisi kama  wadau na watumiaji wazuri wa mtandao,hata shughuli za chuo zinaendeshwa kwa njia ya  mtandao,hivyo ni muhimu kwetu ili tuweze kujilinda na uhalifu wa mtandao,"amesema

 

Naye mtaalam wa usalama mtandao ya uchunguzi wa makosa ya kidigitali,kutoka Wizara hiyo,Yusuph Kileo,amewataka wananchi kutambua kilo mmoja ana jukumu la kujilinda kwenye mtandao,kuhakikisha wanatumia nywila madhubuti ili wabaki salama kwenye mtandao.

 

Amesema moja ya changamoto kubwa ni pamoja na watu wengi kutokuripoti matukio hayo na kuwa chanzo cha wahalifu kuendelea kudhuru wengine.

 

"Tumekuwa tukihamasisha watu wawe makini wanapofanya mambo yao mtandaoni mfano kuangalia taarifa gani wanaweka mtandaoni isije kuwa chanzo cha wao kuwa wahanga wa mtandaoni, tunahamasisha watu wawe na tabia ya kuripoti haya matukio ya uhalifu mtandaoni,"

 



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post
Alert: Content is protected !!