Mashirika ya kijamii wavaa jukum la kutokomeza ukatili wa kijinsia nchini







Bertha Mollel, Arusha .

 

 

Wakati matukio ya ukatili wa kijinsia yakiendelea kutia doa nchini huku Arusha ikitajwa kuongoza mikoa mingine, baadhi ya Mashirika ya Kijamii yameungana kuunda mtandao maalum wa kutokomeza matukio hayo yanayoacha maumivu makubwa kwa waaathirika.

 

Matukio makubwa ya ukatili yanayotajwa nchini ni pamoja na ubakaji, kulawiti, mimba za watoto na ndoa za kulazimishwa.

 

kwa mujibu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk Doroth Gwajima,  kwa mwaka 2022 pekee zaidi ya kesi 12,163 za Ukatili wa Kijinsia yameripitiwa nchini huku waaathirika wakubwa wakiwa ni wanawake (9962) na wanaume ni 2201.

 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mtandao huo jijini Arusha, mwenyekiti Rose Njilo alisema mpango huo  umeratibiwa chini ya ‘Mimutie Women Organization,’ kwa lengo la kuzifikia jamii nyingi za pembezoni na kuwasaidia dhidi ya majanga hayo ya ukatili wa kijinsia.

 

 

 

"Kesi za unyanyasaji wa kijinsia zinatokea zaidi katika jamii za pembezoni  kwa sababu hawana taarifa sahihi za madhara ya matukio haya lakini wengi wao bado hawajui kusoma na kuandika huku wakiwa wamefungwa chini ya Mila na desturi zao," alieleza Bi Njilo.

 

 

 

Mtandao mpya wa kupinga Ukatili wa Kijinsia unaundwa na Mimutie Women Organization (MWO), Embuan Development Organization (EMBUDEO), Dunia Salama Foundation, Media Aid for Indigenous and Pastoralist Community (MAIPAC), Oseremi Development Organization na FOMA.

 

 

 

Njilo alisema wakazi wa Kanda ya Kaskazini hasa Mkoa wa Arusha na Manyara wanaonekana kukumbwa na matukio makubwa ya ukatili wa kijinsia hivyo kuhitaji elimu zaidi ya kuripoti matukio haya, lakini pia namna ya kuepuka viatararishi na matukio haya kutokea.

 

 

 

Alitaja baadhi ya matukio ya Ukatili wa kijinsia kuwa ni unyanyasaji wa kijinsia, ndoa za utotoni na za kulazimishwa, mashambulizi ya kikatili na kushambuliwa kwa majeraha na wakati mwingine vifo pamoja na ukeketaji.

 

 

Njilo alibainisha kuwa mambo mengi ya aina hiyo huwa hayaripotiwi, lakini hivi karibuni mashirika yao yalifanikiwa kupata kesi 17 ambazo zilifikishwa mahakamani na angalau kufanikiwa kushinda  kesi moja ya kisheria zingine zikiwa katika hatua mbalimbali za uendeshaji.

 

 

Ofisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Arusha, Blandina Nkini alisema tafiti zilizofanywa na Serikali zimebaini kuwa matukio mengi ya Ukatili yanasababishwa na imani potofu za kimila na malezi duni.

 

"Kwa sasa tunaelekeza nguvu kwenye kutoa  Elim ya malezi na makuzi bora kwa wazazi ilii kila mmoja atambue na kutekeleza majukumu yake ambayo yataleta watoto wenye maadili baadae watakaokuwa na hofu ya kutekeleza matukio haya ya Ukatili"

 

 

 

Mwisho

 

 

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post
Alert: Content is protected !!