Na Bertha
Mollel , Arusha
Waziri
wa Katiba na Sheria, Dkt Damas Ndumbaro amewaagiza wasaidizi na wataalamu wa kisheria
kutumia mifumo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (Tehama), katika
kutoa misaada ya kisheria ili kuweza kusaidia jamii kubwa kwa haraka na wepesi zaidi.
Waziri
Ndumbaro ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha mafunzo ya matumizi ya mifumo
ya Tehama kwa Wasajili wasaidizi wa huduma za sheria, maafisa magereza,
taasisi za huduma za msaada wa sheria, wataalamu wa sheria na
watumishi kutoka Tamisemi kinachofanyika mkoani Arusha kwa siku mbili.
“Matumizi
ya Tehama yakitumika zaidi katika kutoa elimu au misaada ya kisheria inarahisisha
mambo mengi ikiwemo hata kuokoa mda wa kuzifuata huduma hizo maofisini lakini
pia foleni katika ofisi hizi zitapungua na wananchi kuona faida na umuhimu wenu”
Alisema
wizara yake inasisitiza matumizi ya Tehama pia katika kipindi hiki zaidi
ambacho wananchi wanadai katiba mpya ambayo mifumo hii itasaidia kujua katiba iliyopo, inafanya
nini na ina mapungufu gani na yapi ambayo yanafaa kufanyiwa maboresho.
“Huwezi
kudai katiba mpya bila kujua ina mapungufu gani hivyo hakikisheni wananchi
wanayapata hayo huko huko walipo kwani
wakishajua ndio wataweza kudai haki yao vizuri” alisema Ndumbaro na kuongeza…
“Bajeti
ya mwaka 2022/2023 Wizara yangu imeweka vipaumbele 14, ikiwemo matumizi ya tehema, katika mifumo
yote ya sheria ili matumizi yote yaende kidigitali na niwapongeze watoa huduma
za kisheria mmeanza kutumia”
Waziri Ndumbaro, alisema Mhimili wa mahakama umefanikiwa sana katika matumizi
ya Tehama likifungamanishwa na haki kupatikana kwa haraka na kuondoa
usumbufu.
Awali akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria, Kaimu Katibu tawala mkoa
wa Arusha, David Lyamongi, alisema kuwa Mawakili binafsi wamekuwa ni
msaada mkubwa katika maswala ya kisheria ambapo wamekuwa wakitumika kutatua
kesi mbalimbali kwa wananchi na hivyo kuondoa usumbufu na haki kupatikana
.
Amesema kuwa kupitia mawakili hao Yatima na Wajane wamekuwa wakipata msaada
hivyo umefikawakati wapewe kipaumbele na nguvu ya kisheria ili kuweza kukamilisha
kazi yao kwa wakati.
Nae mkuu wa Kitengo cha Tehama wizarani, Gabriel Omary, amesema mafunzo
hayo ya utumiaji wa huduma ya Tehama yana lengo la kuwezesha wananchi
kutumia huduma ya mtandao ilikuweza kupata haki kwa wakati na haraka ikiwa
ni pamoja na kuwapunguzia gharama pindi wafuatapo huduma za kisheria.
![]() | |
Baadhi ya washiriki wa
|
“leo
tunawanoa zaidi wenzetu wanaotoa misaada ya kisheria katika taasisi mbali mbali
mbali za magereza, uhamiaji, polisi, tamisemi kwa ajili ya kutambua namna ya
kutumia mfumo wa Tehama kusaidia jamii hasa maswala ya kisheria ambapo
tunatarajia wananchi watanufaika nazo”
![]() | |
Baadhi ya washiriki wa
|