NA OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Innocent Bashungwa ametoa maelekezo kwa wakurugenzi wote nchini kuhakikisha vituo vyote vya afya kunakuwa na dirisha la wazee na muda wote kuwe kuna muuguzi ambaye anahakikisha wazee wanapata matibabu bila shida yoyote.
Amesema ifikapo Septemba Mosi,mwaka huu huduma ndogo ndogo zianze kutolewa kwa wananchi waanze kuzipata huku kituo kikiendelea kukamilika.Aidha, amesema kwa majengo mapya ambayo fedha imekuja na bado haijatumika viongozi wamepewa mpaka Desemba kuhakikisha fedha hiyo na majengo hayo mapya yawe yameshakamilika.
Mheshimiwa Bashungwa amesema, Mkuu wa mkoa akifika na kukuta maelekezo hayo bado hayajafanyiwa kazi, basi achukuwe hatua stahiki.Amesema, fedha zinapokuja kwenye maeneo ya kata kwa malengo ya kujenga vituo vya afya viongozi ni jukumu lao kuhakikisha wanasimamia ili kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.