NA Mwandishi wetu.
KLABU
ya Azam FC imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu ujao baada ya
kumsajili Mfungaji Bora wa Azam Sports Federation Cup (ASFC), Abdul
Hamisi Suleiman ‘Sopu’ kutoka Coastal Union kwa mkataba wa miaka mitatu.
Sopu ambae mabosi wake wa zamani Simba SC walianza kumnyatia kuitaka saini yake kwa mazungumzo ya Siri Siri, Yanga nao walionekana kumsumbua usiku kucha katika kambi waliyokuwa wamefikia jijini Arusha Mara baada ya mchezo wa fainali wa kombe la Azam.
Katika mchezo huo licha ya coastal union kushindwa kutwaa kombe lakini Sopu alionekana kuwasumbua vigogo- hao wa soka dakika 120 zote walizocheza Hadi kuwapeleka hatua ya matuta.
Usajili
wa safari hii ukifanywa na mmiliki wa timu mwenyewe, Yussuf Bakhresa
kwa kushirikiana na Mtendaji Mkuu, Abdukkarim Amin (Popat).
kocha mpya wa makipa, raia
wa Hispania, Dani Cadena ambaye amewahi kufundisha klabu za Sevilla na
Real Betis za Hispania na nyingine za China na Asaudi Arabia akiwa na
uzoefu mkubwa na elimu ya juu ya Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA).